Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Abdul-Malik al-Houthi, Katibu Mkuu wa Ansar Allah Yemen, akirejelea jalada linalomhusu Jeffrey Epstein, amesema kuwa nyaraka zilizochapishwa kutoka katika kesi hiyo zimefichua kwa upana kile alichokiita “ibada za kishetani” pamoja na uhalifu wa kutisha dhidi ya watoto na wasichana wadogo.
Amesisitiza umuhimu wa kuzipa uzito nyaraka hizo, akidai kuwa jalada hilo linaweka wazi moja ya chimbuko la kuibuka kwa harakati ya Uzayuni, na kuashiria kuwa baadhi ya viongozi walitokana na mazingira kama hayo.
Al-Houthi ameongeza kuwa nyaraka za Epstein zimebainisha mambo yaliyokuwa yamefichwa kwa muda mrefu, na kufunua sura “za kutisha na za aibu sana.” Kwa mujibu wake, katika ibada hizo walihusika baadhi ya wasomi na wanasiasa wa Magharibi, wakiwemo kutoka United States na United Kingdom, pamoja na baadhi ya matajiri waliokuwa na mienendo potovu.
Your Comment